Maktaba bora

Shule ina maktaba bora yenye vitabu vya kutosha kwa kila somo. pia maktaba yenye mazingira bora na tulivu kwa wanafunzi na walimu kujisomea wakati wowote .

Maabara Ya Kisasa

Shule ina maabara bora sana kwa masomo ya sayansi. pia imejaa vifaa vya kutosha kwa masomo yote matatu ya sayansi physics , Biology na Chemistry

Mazingira Tulivu

Shule inapatikana katika mazingira tulivu sana, yaliyo kimya na yanayofaa kwa watoto wa kike kujisomea

Imani katika Bwana

Shule inawajenga watoto katika imani ya bwana bila kubagua imani ya mtu. pia kumwabudu mungu wakati wote

Maabara bora ya kompyuta

Shule ina maabara bora kabisa yakufundishia Kompyuta ili kuwafanya wanafunzi kuijua teknolojia ili kuendena na maisha ya kisasa na ushindani.

Mitandao ya kijamii

shule inapatikana katika mitandao mbali mbali ya kijamii kama| Facebook kupitia michaud page

Kwanini Michaud ni bora

Waalimu bora

Shule ina waalimu wakutosha, wenye uzoefu wa muda mrefu, pia wenye uwezo mkubwa wa kufaulisha wanafunzi kwa viwango vya juu kwenye mitihani yote ya Ndani ya nje na hasa ya kitaifa kwa kupata daraja la kwanza (Division I)

Ufaulu mzuri katika mitihani ya taifa, ya nje na ya ndani

Shule inafanya vizuri katika mitihani ya taifa kidato cha Pili na Cha nne kwa Miaka yote kwa kufaulisha wanafunzi wote kwa kupata daraja la kwanza Div 1. Pia katika mitihani ya nje, Mock F4, Mitihani ya Kanda pamoja na mitihani ya mkoa

Nidhamu bora ya wanafunzi

Wanafunzi wa Michaud wananidhamu iliyo bora wakiwa nje na ndani ya shule, kwa kuheshimu watu wote bila kujali umri wao na vyeo au nafasi walizonazo pia kijituma katika kazi mbalimbali

Mazingira bora ya kusomea

Shule inapatikana katika mazingira safi na bora yanayo ruhusu na kusaidia watoto wa kike kujisomea kwa utulivu na amani bila kuwa na ushawishi Wanamna yoyote ile.

Je unataka kujiunga na shule yetu iliyo bora Tanzania?

Mawasiliano